Thursday, April 28, 2016

MAN UNITED KUPIGA UZI MWEUPE FAINALI YA FA.


KLABU ya Manchester United imepangwa kuwa timu ya ugenini katika mchezo wa fainali wa Kombe la FA dhidi ya Crystal Palace hivyo kumaanisha kuwa watavaa fula zao nyeupe, kaptura nyeusi na soksi nyeupe Katika Uwanja wa Wembley Mei 21 mwaka huu. Palace wao watakuwa kama wenyeji wa fainali hiyo baada ya kurushwa shilingi hivyo watavaa jezi zao zilizoeleka za nyekundu na bluu. Fulana za fainali ya mwaka huu zitarudisha kumbukumbu ya klabu hizo mbili mara ya mwisho zilizpokutana katika fainali ya michuano hiyo kwenye Uwanja wa Wembley mwaka 1990 wakati United walivyovaa nyeupe dhidi ya rangi zilizoeleka za Palace. Fainali ya mwaka 1990 timu hizo zilitoka sare ya mabao 3-3 baada ya muda wa nyongeza kabla ya kurudiana tena katika uwanja huohuo na United kushinda kwa bao 1-0.

No comments:

Post a Comment