Friday, November 27, 2015

VALBUENA AFUNGUKA KUHUSU BENZEMA NA SAKATA LA MKANDA WA NGONO.

MCHEZAJI wa kimataifa wa Ufaransa, Mathieu Valbuena amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu Mfaransa mwenzake Karim Benzema na tuhuma za ulaghai za mkanda video ya ngono. Valbuena amesema Benzema alipendekeza ingawa moja kwa moja, kuwa awalipe watu waliokuwa wakimpa vitisho ili aweze kuupata mkanda huo. Benzema yuko chini ya uchunguzi akidaiwa kujuhusisha na sakata hilo ingawa mawakili wake wamesisitiza kuwa mteja wao hana hatia. Mkanda unadaiwa kuwa unawahusisha Valbuena na mpenzi wake.

No comments:

Post a Comment