Friday, August 28, 2015

WILFRIED BONY MAJANGA.

MSHAMBULIAJI wa Manchester City, Wilfried Bony anaweza kukaa nje ya uwanja kwa kipindi kirefu zaidi baada ya kutuma picha katika mtandao akiwa na magongo huku mguu wake ikiwa umefungwa bandeji gumu. Bony hajacheza katika mechi yeyote kati ya tatu za Ligi Kuu ambazo City wamecheza msimu huu na sasa anatarajiwa kukosekana kwa muda mrefu zaidi kutokana na picha hiyo aliyotuma. Bony alitua City akitokea Swansea City kwa kitita cha paundi milioni 28 katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo Januari mwaka huu. Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast kwa ujumla amecheza mechi 30 za Ligi Kuu msimu uliopita na kufunga mabao 11.

No comments:

Post a Comment