Friday, August 28, 2015

RUFANI YA PIQUE YATUPILIWA MBALI.

BEKI wa Barcelona, Gerard Pique anatarajiwa kukosa safari ya kwenda kuifuata Atletico Madrid mwezi ujao baada ya rufani yake kupinga adhabu ya kufungiwa mechi nne kutupiliwa mbali jana. Pique alionyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumtolea maneno ya matusi mwamuzi msaidizi wakati Barcelona walipotandikwa kwa jumla ya mabao 5-1 katika mchezo wa Super Cup dhidi ya Athletic Bilbao wiki iliyopita. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania alikuwekwa kando wakati mabingwa hao wa Ulaya walipolipa kisasi kwa Bilbao kwa kuitandika bao 1-0 katika mchezo wao wa kwanza wa La Liga mwishoni mwa wiki iliyopita. Hata hivyo, Pique sasa anatarajiwa kukosa mchezo dhidi ya Malaga utakaochezwa kesho na Levante utakaochezwa Septemba 20 sambamba na ule wa Atletico Septemba 12.

No comments:

Post a Comment