Friday, August 28, 2015

EUROPA LEAGUE DRAW: LIVERPOOL KUANZA NA RUBIN KAZAN, SPURS KUPIGA MASAFA MPAKA AZERBAIJAN.

KLABU ya Liverpool, inatarajiwa kusafiri kwenda Urusi baada ya kupangwa kundi moja na Rubin Kazan katika michuano ya Europa League. Liverpool iliyo chini ya meneja Brendan Rodgers pia wanatarajiwa kupambana na Bordeaux ya Ufaransa na FC Sion ya Uswisi katika kundi lao. Kwa wa Tottenham Hotspurs wao wanakabiliwa na safari ndefu ya kuifuata Qarabag ya Azerbaijan huku pia wakipangwa kucheza na Anderlecht ya Ubelgiji na Monaco ya Ufaransa. 
Celtic ambao waling’olewa katika hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wao watavaana na Ajax Amsterdam ya Uholanzi, Fenerbahce ya Uturuki na Molde ya Norway katika kundi lao. Kila inatarajiwa kucheza mechi sita katika makundi yao huku mechi za kwanza zikitarajiwa kuchezwa Septemba 17 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment