Friday, August 28, 2015

CITY IMEJIPANGA KUMPA MSHAHARA MNONO DE BRUYNE.

MKURUGENZI wa michezo wa Wolfsburg ya Ujerumani Klaus Allofs amedai kuwa Manchester City imejipanga kumpa ofa ya mshahara mkubwa winga wao Keniv de Bruyne. De Bruyne mwenye umri wa miaka 24, ameachwa katika kikosi cha Wolfsburg kitakachopambana na Schalke baadae leo kutokana na kuendelea kwa mazungumzo yake ya kwenda City. Allofs amesema mara ya kwanza walikuwa hawataki kumuuza De Bruyne lakini sasa wameamua kuanza mazungumzo na City ingawa hakuna lililoafikiwa mpaka sasa. City hawajatoa kauli yeyote juu ya taarifa za kukubali kwao kutoa kitita cha paundi milioni 58 kwa ajili ya kumnyakuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji.

No comments:

Post a Comment