Friday, July 31, 2015

VAN DER VAART AITUHUMU MADRID KWA KUKOSA UVUMILIVU.

KIUNGO wa zamani wa Real Madrid, Rafael van der Vaart ameituhumu klabu yake hiyo ya zamani wa kukosa uvumilivu. Kiungo huyo wa kimataifa wa Uholanzi alivaa jezi ya Madrid kuanzia mwaka 2008 mpaka 2010 kabla ya kuondoka na kuhamia Tottenham Hotspurs na anadhani mategemeo makubwa waliyonayo hayaisaidii timu hiyo. Akihojiwa Van der Vaart amesema ukiwa Madrid kama hutashinda chochote lazima utaingia katika matatizo makubwa. Mkongwe huyo aliendelea kudai kuwa kwa maono yake anadhani Madrid hawana uvumilivu kwani ukipoteza mechi moja kwao ni kama duniani inakuwa imeishia hapo.

No comments:

Post a Comment