Sunday, July 5, 2015

MASHABIKI WA ATLETICO HAWATAMSAMEHE DE GEA AKIJIUNGA NA MADRID - UJFALUSI.

BEKI wa zamani wa Atletico Madrid, Tomas Ujfalusi anaamini mashabiki watachukulia uhamisho wa zao lao kutoka timu ya vijana David De Gea kwenda Real Madrid kama dalili za usaliti. De Gea amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia Madrid kipindi hiki cha majira ya kiangazi akitokea Manchester United pamoja na kukuzwa na Atletico toka akiwa na umri wa miaka 13 na kufanikiwa kushinda taji la Europa League pamoja na Super Cup akiwa na kikosi cha kwanza. Akihojiwa kuhusiana na hilo Ujfalusi ambaye ameitumikia timu hiyo kuanzia mwaka 2008 mpaka 2011 amesema kamwe mashabiki wa Atletico hawatamsamehe kama akijiunga na mahasimu wao Madrid. Beki huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech pia amedai anashangazwa na taarifa hizo kwani anamfahamu De Gea kuwa mshabiki wa Atletico toka akiwa na umri mdogo hivyo utakuwa sio uamuzi rahisi kuchukua.

No comments:

Post a Comment