Friday, July 31, 2015

GUARDIOLA MGUU NDANI MGUU NJE BAYERN.

MENEJA wa Bayern Munich, Pep Guardiola amesema hatasaini mkataba mpya na klabu hiyo mpaka atakapojiridhisha kuwa ni jambo la busara kwa pande zote mbili. Kumekuwa na tetesi zilizoibuka juu ya mustakabali wa kocha huyo ambaye mkataba wake unamalizika mwakani huku taarifa zingine zikidai tayari ameshakubali kuhamia Manchester City. Guardiola mwenye umri wa miaka 44, hajathibitisha mipango yake lakini amekiri kuwa hana uhakika kama ataendelea kuwepo Allianz Arena. Akizungumza na wanahabari, Guardiola amesema kwasasa yeye ni kocha wa Bayern na anafurahia hilo lakini bado hajaamua kuhusu mustakabali wake na pindi atakapopata uamuzi atawaarifu Kalle Rummenigge ambaye ni rais, Mathias Sammer mkurugenzi wa michezo na Uli Hoeness ambaye ni rais wa zamani wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment