Friday, May 22, 2015

RODGERS AMTAKA STERLING KUMALIZA MKATABA WAKE.

MENEJA wa Liverpool, Brendan Rodgers amesema anategemea Raheem Sterling kumaliza miaka miwili ya mkataba wake uliobakia pamoja na msuguano uliopo kati ya mchezaji huyo na klabu kuhusu mkataba mpya. Wakala wa Sterling, Aidy Ward amesisitiza jana kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 hatabakia Anfield hata kama akipewa ofa ya kulipwa kitita cha euro milioni 1.3 kwa wiki. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo Rodgers amesema in vigumu kuzungumzia kilichosemwa na wengine kwani mkutano wowote unaofanyika katika klabu hiyo mambo yake hubakia kuwa siri. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kama kutakuwa na mazungumzo au la, Sterling bado ana mkataba wa miaka miwili na anategemea nyota huyo ataheshimu hilo. Rodgers amesema haoni kama Sterling hana furaha, hivyo anategemea kuendelea kumtumia katika mchezo wao wa mwisho wa ligi msimu huu utakaofanyika Jumapili hii.

No comments:

Post a Comment