Tuesday, April 21, 2015

SMALLING AKUBALI KUSAINI MKATABA MPYA NA UNITED.

BEKI wa klabu ya Manchester United, Chris Smalling amekubali kusaini mkataba mpya ambao utambakisha katika timu hiyo mpaka June mwaka 2019. Smalling mwenye umri wa miaka 25 alijiunga na United akitokea Fulham mwaka 2010 na ameshinda mataji mawili ya Ligi Kuu akiwa Old Trafford. Akihojiwa meneja wa United, Louis van Gaal amesema Smalling ameimarika na amekua kwa kipindi kifupi ambacho amekuwa akiinoa timu hiyo. Van Gaal aliendelea kudai kuwa beki huyo amekuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo na amefurahi kusaini mkataba mpya.


No comments:

Post a Comment