Sunday, February 1, 2015

COSTA ADAI KUTOMKNYGA KWA MAKUSUDI CAN.

MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa amesema hakuwa na nia yeyote ya makusudi kumkanyaga mchezaji wa Liverpool Emre Can. Chama cha Soka Uingereza-FA kilimtwanga adhabu kwa vurugu kutokana na tukio hilo lililotokea katika mchezo wa nusu fainali ya mkondo wa pili wa Kombe la Ligi Jumanne iliyopita jambo ambalo Costa amelipinga. Costa mwenye umri wa miaka 26 amesema jambo kubwa ni wakati akienda nyumbani kwake kulala na kujua kuwa hakufanya jambo lolote baya. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amesema hakuwa na nia ya makusudi kutenda kitendo kile kwani ilikuwa bahati mbaya. Costa amesema amekubali ns kuheshimu adhabu aliyopewa lakini amesisitiza hakufanya vile kwa makusudi.

No comments:

Post a Comment