Friday, November 21, 2014

UEFA KUTOA MSIMAMO WAKE DESEMBA 4 KUHUSIANA NA TIMU ZA CRIMEA.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA, Michel Platini amesema shirikisho hilo litafanya uamuzi wa kama watatambua michezo ya vilabu kutoka Crimea chini uangalizi wa Shirikisho la Soka Urusi-RFU Desemba 4 mwaka huu. Klabu tatu za Crimea ambazo ni TSK Simferopol, SKChF Sevastopol na Zhemchuzhina Yalta zimekubaliwa kucheza katika ligi ya ubingwa ya Urusi kufuatia matatizo ya kisiasa katika eneo lao. Shirikisho la Soka la Ukraine-FFU lilikata rufani Shirikisho la Soka Duniani-FIFA na UEFA kutoa adhabu kwa RFS kwa kile walichokiita kufuruga sheria za soka. UEFA ilifanya kikao na RFS na FFU katika makao makuu yake jijini Nyon Septemba mwaka huu na pande zote zilikubaliana kuundwa kwa kikosi kazi kutafuta suluhu katika suala hilo. Platini alikaririwa katika mtandao wa UEFA akidai kuwa kikosi kazi kilichoundwa kinatafuta suluhu katika suala hilo na uamuzi wa mwisho utatolewa mapema mwezi ujao.

No comments:

Post a Comment