Friday, November 21, 2014

SAMMER AONGEZWA MIAKA MITATU BAYERN.

KLABU ya Bayern Munich imetangaza kumuongeza mkataba wa miaka mitatu zaidi mkurugenzi wa michezo wa timu hiyo Matthias Sammer ambao utamalizika mwaka 2018. Sammer ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Ujerumani na kocha, alijiunga na Bayern mwaka 2012 akitokea Shirikisho la Soka la Ujerumani ambako nako alikuwa mkurugenzi wa michezo. Akihojiwa na wanahabari Sammer amesema miaka miwili na nusu ambayo ameitumikia klabu hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kwani walifikia malengo yao mengi waliyojiwekea. Toka atue Bayern, Sammer amefanikiwa kuisaidia timu hiyo kushinda taji la Bundesliga katika msimu wa 2013-2014, Kombe la Ligi sambamba na taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya 2013.

No comments:

Post a Comment