Friday, November 21, 2014

NADAL AMUOSHESHA VYOMBO RONALDO BAADA YA KUMFUNGA KATIKA KARATA.

MCHEZAJI nyota wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Ronaldo amelazimika kuosha vyombo baada ya kushindwa katika mchezo wa karata na mchezaji tenisi nyota kutoka Hispania Rafael Nadal. Katika mchezo huo Nadal alipokea kitita cha dola 50,000 katika mfuko wake wa misaada huku Ronaldo akiosha vyombo baada ya kushindwa. Mchezo huo ulikuwa maalumu kwa ajili ya hafla ya chakula kilichoandaliwa katika Casino ya Hippodrome jijini London, Uingereza. Kitendo cha Ronaldo kukubali kuosha vyombo alivyokuwa ametumia Nadal wakati wa kula kiliwafurahisha wageni waalikwa katika hafla hiyo mahsusi.

No comments:

Post a Comment