Thursday, October 30, 2014

WINGA WA CELTIC AFUNGIWA MECHI SABA KWA UBAGUZI.

WINGA mahiri wa klabu ya Celtic, Aleksandar Tonev amefungiwa mechi saba kwa kosa la kumfanyia vitendo vya unaguzi wa rangi beki wa timu ya Aberdeen Shay Logan. Tonev mwenye umri wa miaka 24 alilimwa adhabu hiyo kufuatia tukio hilo na Logan ambaye ni raia wa Uingereza katika mechi ya Ligi Kuu nchini Scotland Septemba mwaka huu. Winga huyo wa kimataifa wa Bulgaria yuko kwa mkopo Celtic akitokea klabu ya Aston Villa. Celtic katika taarifa yake wamesema watakata rufani kupinga adhabu hiyo wakidai kuwa mchezo huyo siyo mbaguzi. Tukio hilo limetokea katika kipindi cha cha mchezo ambao Celtic waliifunga Aberdeen mabao 2-1 Septemba 13.

No comments:

Post a Comment