Thursday, October 30, 2014

VILABU VIKUBWA ULAYA KUKUTANA KUJADILI MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA 2022 QATAR.

KLABU kubwa barani Ulaya zinatarajiwa kukutana wiki ijayo ili kutoa ombi kwa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuruhusu michuano ya Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar kuchezwa kati ya Aprili 28 na Mei 29 wakati huo. Qatar ilishinda haki ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2010 lakini kumekuwa na tume maalumu iliyoundwa kuangalia uwezekano wa michuano hiyo kuchezwa majira ya baridi kutokana na joto kali lililopo katika nchi hiyo majira ya kiangazi. Muungano wa vilabu vya Ulaya-ECA, ambao unajumuisha vilabu vya Manchester, Liverpool, Barcelona na Bayern Munich unataka kuwasilisha ombi hilo ikiwemo kuanza mechi za ligi ya msimu wa mwaka 2021-2022 wiki mbili mapema na kucheza mechi za mwisho za kombe la FA baada ya fainali hizo. Kama FIFA wakiruhusu michuano hiyo kuchezwa kipindi hicho, hatua hiyo itasababisha Kombe la FA la Uingereza kukamilika Juni. Muungano huo unaowakilisha timu 214 za bara Ulaya, unaamini muda huo huenda ukaathiri pia mashindano ya mataji ya nyumbani kwa nchi za Ufaransa na Hispania.

No comments:

Post a Comment