Friday, October 24, 2014

VAN GAAL AMPA SHAVU VALDES.

KLABU ya Manchester United imetangaza kuwa golikipa wa zamani wa klabu ya Barcelona, Victor Valdes anatarajiwa kuanza kufanya nao mazoezi. Valdes mwenye umri wa miaka 32 ambaye aliondoka Barcelona mwishoni mwa msimu uliopita baada ya kuitumikia timu hiyo katika kipindi chake chote kwasasa bado anapona majeruhi ambayo yalisababisha kushindwa kujiunga na Monaco ya Ufaransa. Golikipa huyo ambaye amecheza mechi 20 za kimataifa akiwa na Hispania aliumia goti lake la kulia Machi mwaka huu na kfanyiwa upasuaji ambao ulimuweka nje kwa msimu uliobakia pamoja na Kombe la Dunia. 
Valdes akiwa na Van Gaal mwaka 2002 katika mazoezi ya Barcelona.
Meneja wa United, Louis van Gaal amempa ofa Valdes nafasi ya kufanya mazoezi na kuhakikisha anapona kabisa goti lake katika timu hiyo. Katika taarifa ya klabu hiyo imedai kuwa Valdes ambaye ni mchezaji huru atakuwa akifanya mazoezi chini ya uangalizi wa madaktari wa United ili kuhakikisha anapona kabisa. Van Gaal ndiye aliyempa nafasi ya kucheza kwa mara ya kwanza Valdes wakati akiwa na umri wa miaka 20 mwaka 2002 lakini alikaa naye kwa kipindi cha miezi sita kabla ya kocha huyo hajaondoka Barcelona.

No comments:

Post a Comment