Friday, October 24, 2014

KAMA KAWAIDA YAKE, BALOTELLI MATATANI TENA.

POLISI wanachunguza madai kuwa mshambuliaji nyota wa Liverpool, Mario Balotelli wamemtishia mwanamke ambaye alikuwa akipiga picha gari lake la kifahari aina ya Ferrari. Inadaiwa mwanamke anamtuhumu nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 kumfuata binti yake ambaye alikuwa akilipiga picha gari hilo lililokuwa limeegeshwa pembeni. Polisi wa Manchester wamedai kupokea taarifa ya tishio na wanafanya uchunguzi kwa kuwahoji watu mbalimbali ambao walikuwa karibu na eneo hilo. Balotelli ameendelea kuandamwa na matukio baada ya juzi kupokea onyo kutoka katika kllabu yake kwa kubadilishana shati na beki wa Real Madrid Pepe wakati timu yake ikiwa nyumba kwa mabao 3-0 katyika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uliofanyika katika Uwanja wa Anfield.

No comments:

Post a Comment