Thursday, October 30, 2014

JUVENTUS KUIVAA NAPOLI JIJINI DOHA KATIKA MCHEZO WA SUPERCUP.

MAOFISA wa Serie A nchini Italia wamethibitisha kuwa mtanange wa Supercup ambao utawakutanisha mabingwa wa ligi hiyo Juventus na mabingwa wa Kombe la Italia Napoli, utafanyika jijini Doha, Qatar Desemba 22 mwaka huu. Hii itakuwa mara ya saba kwa mtanange huo kufanyika nje ya Italia na waandaaji wanategemea mchezo wa kiungwana kuliko uliozikutasha timu hizo jijini Beijing miaka miwili iliyopita. Katika mechi hiyo Juventus walishinda kwa mabao 4-2 baada ya muda wa nyongeza huku wachezaji wawili wa Napoli wakipewa kadi nyekundu na baadae kukataa kuzungumza na wanahabari. Supercup ilianza kuchezwa nje ya Italia mwaka 1993 wakati AC Milan ilipokwaana na Torino jijini Washington, baadae ilikwenda nchini Libya mwaka 2002 na kurejea tena Marekani kwa kuchezwa katika Uwanja wa Giants mwaka 2003. Mtanange huo pia umewahi kuchezwa jijini Beijing mwaka 2009 na 2011.

No comments:

Post a Comment