Wednesday, October 29, 2014

DORTMUND YASIMAMISHA MAZUNGUMZO YA MKATABA NA REUS.

MKURUGENZI wa michezo wa Borussia Dortmund, Michael Zorc amekiri kusimamisha mazungumzo ya mkataba mpya na Marco Reus ili kuweka mkazo katika kiwango chao uwanjani. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani ana mkataba na Dortmund unaomalizika kiangazi mwaka 2017 lakini kuna kipengele kinachomuwezesha kuondoka kama klabu inayomtaka itatoa kitita cha euro milioni 25 mwishoni mwa msimu huu. Dortmund walikuwa wakitaka kumuongeza Reus mkataba mwingine bila kuweka kipengele cha cha kuuzwa huku Bayern Munich nao wakimfuatilia nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 kwa karibu. Kwa sasa Dortmund wanaonolewa na Jurgen Klopp wako katika nafasi ya 15 katika msimamo wa Bundesliga wakiwa wameambulia alama saba katika mechi tisa walizocheza. Zorc amesema wamesimamisha mazungumzo hayo kutokana na hali ilivyo sasa katika timu hiyo kwani wanataka kutoka katika wakati mgumu waliokuwa nao.

No comments:

Post a Comment