Tuesday, August 19, 2014

NIMEKOMA SING'ATI TENA - SUAREZ.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Barcelona, Luis Suarez amesema mazungumza na mtaalam kuhusu tabia yake na kusisitiza kuwa hatafanya tukio kama hilo tena. Suarez kwasasa anatumikia adhabu ya kufungiwa miezi minne kwa kung’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la Dunia likiwa ni tukio lake la tatu. Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay amesema kuwa amezungumza na daktari wake wa ushauri na akamwelekeza inabidi akubali kosa na kuomba radhi suala ambalo amefanya na sasa anaganga yajao. Suarez mwenye umri wa miaka 27 amesema alipatwa na huzuni baada ya tukio alilofanya nchini Brazil lakini anashukuru suala hilo kwasasa liko nyuma yake na anasonga mbele kuona jinsi atakavyoisaidia timu yake mpya wa Barcelona.

No comments:

Post a Comment