Monday, July 28, 2014

SINA HARAKA YA KUZIBA NAFASI YA SUAREZ - RODGERS.

MENEJA wa Liverpool, Brendan Rodgers amesisitiza hawatakuwa na haraka ya kununua mshambulliaji mpya kuziba nafasi ya Luis Suarez baada ya uhamisho wa Loic Remy kutoka Queens Park Rangers kwenda Anfiled kushindikana. Uhamisho huo wa euro milioni 10 ulikuwa kama umekamilika na Remy alisafiri kwenda nchini Marekani kufanyiwa vipimo vya afya lakini matatizo yaliyogundulika wakati wa vipimo yakasababisha Liverpool kuacha kumsajili. Rodgers sasa amebakiwa na Daniel Sturridge na Rickie Lambert kama washambuliaji pekee anaowategemea lakini kocha huyo amesema hata kuwa na haraka ya kutafuta mshambuliaji mwingine. Akihojiwa mara baada ya Liverpool kuichabanga Olympiakos kwa bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa huko Chicago, Rodgers amesema kuna baadhi ya maeneo anahitaji kuyaboresha katika kikosi chake lakini hajapata wachezaji anahitaji pamoja na kuwa na fedha ya kutosha. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kama itamaanisha kusubiri mpaka Januari ili aweze kupata mchezaji anayehitaji atasubiri lakini hawezi kufanya haraka ya kusajili kwasababu fedha zipo.

No comments:

Post a Comment