Monday, July 28, 2014

NYONGA YAMRUDISHA RAFAEL UINGEREZA.

BEKI wa klabu ya Manchester United, Rafael amerejea nchini Uingereza kwa ajili ya matibabu kutokana na majeruhi ya nyonga. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil aliumia wakati wa mazoezi jijini Denver kuelekea katika mchezo wao walioshinda mabao 3-2 dhidi ya AS Roma. Rafael ambaye kuna uwezekano asicheze tena katika mechi za kujipima nguvu kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi, kurejea kwake nyumbani kunaweza kumpa nafasi ya kupona kwa wakati na kuelendelea na maandalizi mengine timu hiyo itakaporejea. United itafungua pazia la Ligi Kuu kwa kucheza na Swansea City katika Uwanja wa Old Trafford Agosti 16 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment