Saturday, July 26, 2014

LIVERPOOL YAZIDI KUIBOMOA SOUTHAMPTON.

BEKI mahiri wa klabu ya Southampton, Dejan Lovren anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya Liverpool mwishoni mwa wiki hii baada ya klabu hiyo kufikia makubaliano ya kumnunua kwa paundi milioni 20. Beki huyo wa kimataifa wa Croatia mwenye umri wa miaka 25 ambaye alicheza mechi zote za Kombe la dunia akiw ana nchi yake, amewahi kuzungumza waziwazi nia yake ya kujiunga na Liverpool. Lovren anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya katika Uwanja wa Anfield kabla ya Liverpool hawajarejea kutoka katika ziara yao nchini Marekani. Kocha wa Southampton Ronaldo Koeman alithibitisha kuwa Liverpool wanakaribia kumsajili Lovren na kazi yao kwasasa ni kuhakikisha wanapata mbadala wake haraka. Lovren aliyejiunga na Southampton akitokea Lyon kwa ada ya paundi milioni 8.5 katika kipindi cha kiangazi mwaka jana ataondoka Saint Mary akiwa ametumikia miezi 12 ya mkataba wake wa miaka minne aliokuwa nao.

No comments:

Post a Comment