Saturday, July 26, 2014

AJALI YA NDEGE YA ALGERIA YAPELEKEA LIGI KUAHIRISHWA HUKO BURKINA FASO.

WIZARA ya michezo ya Burkina Faso imeahirisha ratiba ya Ligi Kuu nchini humo kufuatia ajali mbaya ya ndege ya Air Algeria iliyotokea Alhamisi iliyopita. Mechi ya 30 na ya mwisho ya ligi ilikuwa imepangwa kuchezwa Jumamosi hii lakini wachezaji na mashabiki walitaarifiwa kupumzika majumbani kwao. Kwa mujibu wa ratiba mpya iliyotolewa na Shirikisho la Spoka la nchi hiyo, timu zitalazimika kusimama kwa dakika moja ili kuwakumbuka watu waliokufa katika ajali hapo kesho. Taarifa zinadai kuwa abiria wote 116 waliokuwemo ndani ya ndege hiyo walifariki dunia katika ajali hiyo huku mamlaka za ndani zikidai 24 kati ya abiria hao walikuwa raia wa Burkina Faso.

No comments:

Post a Comment