Thursday, April 24, 2014

ROBBEN AISHANGAA BAYERN.

WINGA mahiri wa klabu ya Bayern Munich, Arjen Robben ameshangawa na mchezo wa tahadhari waliokuwa wakicheza Real Madrid katika mchezo wao wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Pamoja na Madrid kushinda bao 1-0 katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Santiago Bernabeu, Bayern ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo walimiliki sehemu kubwa ya mchezo huo kwa asilimia 72. Akihojiwa Robben amesema alitegemea mengi zaidi kutoka kwa Madrid lakini badala yake walikuwa wakiwasubiri na kuwaacha watawale mchezo. Katika mchezo huo Karim Benzema ndiye aliyefunga bao pekee lakini ilibakia kidogo Mario Gotze na Thomas watasawazishe baada ya kukosa kufunga katika nafasi za wazi walizopata. Timu hizo zinatarajiwa kurudiana tena Jumanne ili kutafuta mshindi atakayekwenda kwenye fainali itakayofanyika jijini Lisbon, Ureno.

No comments:

Post a Comment