Thursday, April 24, 2014

PLATINI AZIKINGIA KIFUA PSG NA MAN CITY.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Ulaya, Michel Platini amesisitiza kuwa Paris Saint-Germain-PSG na Manchester City hazitafungiwa kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kama wakikutwa na hati ya kukiuka sheria ya matumizi ya fedha. Bodi ya UEFA inayosimamia sheria hiyo imekutana mapema mwezi huu kufanya uchunguzi wa timu zilizokiuka sheria hiyo ambapo mbali na PSG na City vipo pia vilabu vingine 76. Bodi hiyo inatarajiwa kutangaza matokeo ya uchunguzi wake mapema mwezi ujao lakini Platini tayari ameweka wazi kuwa PSG na City hazitaondolewa katka michuano hiyo. Platini amesema kutakuwa na adhabu kali kwa timu zilizokiuka sheria hiyo lakini hakuna yoyote itakayoondolewa katika michuano ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment