Thursday, April 24, 2014

JUVENTUS, BENFICA HAPATOSHI EUROPA LEAGUE.

BAADA ya kumalizika kwa mechi za mkondo wa kwanza za nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa jana, leo kuna uhondo mwingine wa michuano ya Europa League ambapo viwanja viwili vitawaka moto. Katika mechi za leo Juventus maarufu kama vibibi watakua ugenini kupepetana na Benfica ya Ureno katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali. Nusu fainali nyingine ya michuano hiyo inatarajiwa kuzikutanisha timu za Hispania ambapo Sevilla watakuwa nyumbani kuwakaribisha Valencia. Fainali ya michuano hiyo inatarajiwa kupigwa huko jijini Turin katika Uwanja wa Juventus Mei 14 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment