Thursday, April 24, 2014

HATIMAYE JANUZAJ ACHAGUA KUITUMIKIA UBELGIJI.

WINGA wa klabu ya Manchester United, Adnan Januzaj ameamua kuiwakilisha Ubelgiji katika michuano ya soka ya kimataifa. Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots ametangaza katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter amefurahishwa na uamuzi uliochukuliwa na mchezaji huyo. Januzaj amezaliwa jijini Brussels akiwa na wazazi wenye asili ya Kosovo na Albania na kujiunga na United mwaka 2011. Kinga huyo mwenye umri wa miaka 19 alikuwa na nafasi ya kuzichezea nchi za Kosovo, Albania, Turkey, Serbia na hata Uingereza lakini sasa anaweza kuwemo katika kikosi cha Ubelgiji kitakachoshiriki Kombe la Dunia. Kikosi kamili cha wachezaji 30 wa Ubelgiji kinatarajiwa kutajwa Mei 13 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment